Sunday, January 6, 2019

JINSI YA KUTUMIA MATAKWA YAKO ILI KUVUTIA UTAJIRI.


Katika kutumia sayansi ya kupata utajiri, hupaswi kutumia matakwa yako kwa kitu chochote kilichopo nje yako. Usitumie nguvu ya matakwa yako kuwaendesha wengine kama unavyotaka wewe.


Sayansi ya kupata utajiri haitaki wewe uingilie maisha ya wengine, na pale unapofanya hivyo, kwa kutumia matakwa yako kuingilia maisha ya wengine, unaharibu mfumo mzima unaopaswa kutengeneza utajiri kwako. Kadiri unavyohangaika na ya wengine, ndivyo unavyopoteza ya kwako.



Tumia nguvu ya matakwa yako katika kufikiri na kutenda kwa namna ambayo itakuwezesha wewe kupata kile unachotaka. Na katika kuweka nguvu ya matakwa yako kwenye kupata utajiri, usijihusishe kwa namna yoyote na umasikini, usiufikirie umasikini, usitake kujua kwa nini watu ni masikini na wala usisome au kusikiliza vitu vinavyoeleza kuhusu umasikini. Ukatae umasikini kabisa na fikra zako zielekeze kwenye namna bora ya kufikiri ili kutengeneza utajiri.

No comments:

Post a Comment