Tuesday, January 8, 2019

AFYA

Afya ndiyo mtaji wa kwanza na muhimu sana kwenye maisha yetu, bila ya afya bora na imara huwezi kufanya chochote kikubwa kwenye maisha yako. Afya unaweza kuichukulia kirahisi sana unapokuwa nayo, lakini ukishaipoteza gharama zake ni kubwa sana.

KULA VYAKULA vya kiafya kwa kuepuka sukari, kupunguza wanga na kuongeza zaidi mbogamboga, matunda, mafuta na protini. Sumu namba moja kwenye afya zetu ni wanga na sukari, ukiweza kudhibiti hili utakuwa na afya bora.
KUFANYA MAZOEZI, kila siku fanya mazoezi ya kukimbia kwa angalau nusu saa. Mazoezi ya kukimbia ni mazoezi bora kabisa na yasiyo na gharama kwako. Hakikisha unafanya haya kila siku.
KUPUMZIKA, pata muda wa kutosha wa kulala kulingana na uhitaji wa mwili wako. Kwa wastani binadamu tunahitaji masaa 6 mpaka 8 ya kulala kwa siku. Jua mwili wako unahitaji kiasi gani na kila siku upe muda huo. Hili litakufanya uwe imara na kuweza kuweka juhudi kwenye shughuli zako.

No comments:

Post a Comment