Tuesday, January 8, 2019

HEKIMA.

Bila ya hekima, fedha na afya tunazopigania kuwa nazo, zitatupoteza kabisa. Hekima ndiyo inayotuongoza vizuri kwenye maisha yetu, ndiyo inayotuwezesha kufanya maamuzi sahihi kwetu ambayo yanafanya maisha yetu yawe bora zaidi.
KUSOMA; kila siku ya maisha yako, soma angalau kwa dakika 30, na soma vitabu vinavyoongeza maarifa na uelewa wako kwenye kile unachofanya na hata maisha kwa ujumla. Tenga na linda sana muda huu wa kujisomea, ndiyo utakaokutoa hapo ulipo sasa na kukufikisha mbali zaidi.
UZOEFU WA WENGINE; chagua watu ambao utajifunza kupitia wao, hawa tunawaita menta. Unapaswa kuwa na mtu ambaye unataka kufikia hatua ambazo amefikia yeye, kisha kujifunza kila kitu kuhusu yeye. Kama yupo hai na yupo karibu unaweza kutafuta nafasi ya kuonana naye. Na kama yupo mbali huwezi kumfikia au alishafariki basi jifunze kupitia maandiko yake na hata maandiko yaliyoandikwa kuhusu wewe. Mazuri aliyofanya na pia jifunze makosa aliyoyafanya ili uweze kuyaepuka.
KUTAFAKARI; Unapaswa kuwa na muda wako mwenyewe, muda wa kutafakari, kuyatafakari maisha yako na kutafakari kila unachofanya, kuanzia ulikotoka, ulipo sasa na kule unakokwenda. Kila mwisho wa siku yako tafakari kila hatua uliyochukua kwenye siku hiyo na angalia wapi umefanya vizuri, wapi umekosea na wapi unahitaji kurekebisha na kuboresha zaidi. Majibu ya maswali mengi uliyonayo kuhusu maisha tayari unayo, ni wewe kutafakari na kujisikiliza na utapata majibu mengi sana.

No comments:

Post a Comment