Friday, January 4, 2019

EPUKA KAULI HII MWAKA MPYA 2019, " FEDHA SIYO KILA KITU " ILI UWE WA MAFANIKIO MAKUBWA KIFEDHA KWAKO.

Usemi huu ni maarufu sana kwa wengi, hasa masikini, kwamba usijisumbue sana na fedha kwa sababu fedha siyo kila kitu. Hii kauli siyo sahihi kwa asilimia 100, ni kweli kuna vitu muhimu kwenye maisha ambavyo tunavipata bura, kama hewa tunayopumua. Lakini ukiwa mgonjwa na huwezi kuvuta hewa mwenyewe, utauziwa hewa hiyo kwa bei ya juu sana.
Usitumie kauli hii ya fedha siyo kila kitu, kiri kwamba fedha ina mchango mkubwa sana kwenye maisha yako na kazana kuipata ili maisha yako yawe bora.
Vitu kama mahusiano yako na wengine unaweza kuona havihitaji fedha, lakini unapokuwa huna fedha ndiyo unagundua ni vigumu kiasi gani kuendesha mahusiano yako na wengine.

No comments:

Post a Comment