Friday, January 4, 2019

EPUKA KAULI HII MWAKA MPYA 2019 , " KAZI YA FEDHA NI MATUMIZI / KUTANUA / PONDA MALI KUFA KWAJA " ILI UWE NA MAFANIKIO MAKUBWA KIFEDHA KWAKO.

Hivi ndivyo wengi wanavyotengeneza mahusiano yao na fedha, wakizipata watazitumia mpaka ziishe ndiyo waweze kutulia.
Hupaswi kutumia kila fedha unayoipata mpaka iishe, na kwa hakika unapaswa kuweka akiba na kuwekeza kabla hata hujaanza kutumia fedha uliyonayo.
Acha kujiambia kazi ya fedha ni matumizi, au kutumia kauli kama tumia fedha ikuzoee. Kila fedha unayopata weka fungu fulani pembeni kwa ajili ya akiba na uwekezaji kabla hujaanza kutumia.

No comments:

Post a Comment