Tuesday, January 8, 2019

UTAJIRI.

Fedha ni sehemu muhimu sana ya maisha yetu, ukiondoa pumzi ambayo kila mtu anaipata bure, kila kitu kinahitaji fedha. Na hata hiyo pumzi unapoumwa inaacha kuwa bura na unaanza kuilipia. Fedha ni hitaji muhimu sana kwenye maisha yetu, kwa sababu ndiyo inatuwezesha kupata kila tunachotaka.
KIPATO; ongeza kipato chako kwa kutoa thamani zaidi, kujituma zaidi na kuwafikia wengi zaidi. Kama umeajiriwa tekeleza majukumu mengi zaidi na magumu zaidi. Kama unafanya biashara wafikie wateja wapya na wengi zaidi. Fanya zaidi ya ulivyozoea kufanya huko nyuma na kipato chako kitaongezeka.
MATUMIZI; Dhibiti sana matumizi yako, peleka fedha zako kwenye yale mambo ambayo ni muhimu pekee kwenye maisha yako, kama kitu siyo muhimu, achana nacho. Matumizi huwa yana tabia ya kukua kadiri kipato kinavyokua, usipoyadhibiti yatakurudisha nyuma.
UWEKEZAJI; Hutakuwa na nguvu za kufanya kazi kama unavyofanya sasa  miaka yako yote. Hivyo unahitaji kuifanya fedha yako ikufanyie kazi na kukiingizia kipato. Na hapa ndipo uwekezaji unapokuwa muhimu. Weka akiba na wekeza akiba hiyo kwenye maeneo ambayo yanazalisha zaidi kwa baadaye.

No comments:

Post a Comment