Saturday, January 26, 2019

VITABU VIZURI VYA KUSOMA.

  1. )The Law of Success – Napoleon Hill. Nimejifunza na nafanyia kazi suala la kuweka lengo kuu la maisha (definite chief aim).
  2. You’re born an original, don’t die a copy – John Mason. Kubwa ninalofanyia kazi kutoka kitabu hiki ni namna ya kufanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi wakati wote. Mason anasema hatma ya mwanadamu imo katika maamuzi anayoyafanya
  3. Goals – Brian Tracy. Ananifundisha kuwa, malengo lazima uyaandike kila siku bila kuacha hata siku moja. Pia kuwa na dira (vision) ya maisha yangu. Yaani ule kutazama miaka mingi mbele kwa yale unayotaka yatokee na kufanya vitu fulani sasa vinavyokupeleka kwenye ile picha kubwa ya maisha unayoyajenga.
  4. Timiza Malengo Yako – Joel Arthur Nanauka. Nanauka ananifundisha kuwa, kwenye uwekaji malengo, pamoja na kuhakikisha kwamba yako SMART na yameandikwa, lakini lazima lengo kubwa kiasi cha kwamba ukiwaamba watu wakucheke, wahisi umechanganyikiwa. Kama hujachekwa na kushangawa, lengo bado halijawa kubwa ipasavyo. Pia lengo lazima liwekewe mpango wa utekezaji
  5. The magic of thinking $uccess – Dr. David J. Schwartz. Kitabu hiki kinanifundisha kuwa, mafanikio katika jambo lolote yanaanza kwanza kwa kujua kwa hakika kwamba ni nini unahitaji kwenye jambo hilo. Kama hujui unakokwenda, huwezi kufika wala huwezi kupotea. Safari pia haitakuwa na maana. Ndiyo maana lazima kwanza ujue unachohitaji, kisha mengine yafuate.
  6. A setback is a setup for a comeback – Willie Jolley. Katika kitabu hiki, nilijifunza kuwa, fursa yoyote ile imefungashwa kwenye changamoto. Hakuna fursa ya waziwazi, zote zinafikiwa kwa kuingilia mlango unaotwa changamoto.
  7. The impossible is possible – John Mason. Mason katika kitabu hiki ananifundisha kujipambanua. Yale wengine wanayosema hayawezekani, mimi nayafanya. Ni marufuku kufuata mkumbo. Tai huruka peke yao, lakini kunguru huruka katika makundi.
  8. The Power of your subconscious mind – Dr. Joseph Murphy. Nilijifunza kuwa, subconscious mind (akili isiyofikika) ni kama shamba. Usipopanda mazao ya kuliwa, yataota magugu au mimea mwitu. Subconscious mind haiwezi kukaa bure. Kwa hiyo kila mwanadamu (kwa kujua ama kutokujua; kwa kukusudia au kutokukusudia) anapanda mbegu (mawazo) kwenye subconscious mind yake kila siku kwa kadri ya mwelekeo wa tabia zake kimawazo. Hivyo apandacho mtu (kwenye subconscious mind yake), ndicho avunacho kwenye matokeo ya nje. Ili subconscious mind ituhudumie kwa usahihi, lazima tuilishe kwa usahihi pia. Mbegu zetu sasa (mawazo) na ziwe amani, furaha, matendo ya haki, nia njema na mafanikio.
  9. As a man thinketh – James Allen. Namheshimu sana Allen. Kwa ufupi kabisa, nimejifunza kuwa Hali ya nje ya mtu kimazingira, ni dhihiriko la hali yake ya ndani kimawazo. nakazana kuwaza kwa usahihi na najifunza kila siku ili kuboresha hali yangu ya ndani kwanza ili nichochee ubora wa hali yangu ya nje kimazingira.
  10. The science of getting rich – Wallace D. Wattles. Huu ni msaafu wangu wa kuongoza maisha. Ujumbe nilionao kutoka kwenye kitabu hiki ni kuwa, utajiri unapatikana kwa sayansi kamili kama zilivyo sayansi zingine – siyo ajali, bahati wala uchawi wowote. Kikubwa ni kuwaza kwa namna Fulani na kuweka mawazo hayo kwenye vitendo. Dunia haijawahi kupungukiwa na chochote. Hivyo yatupasa tuwaze katika utele, siyo katika uhaba. Fursa za mafanikio hazina kikomo, hakuna mtu mmoja (na pengine hatatokea) wa kumzuia mwingine kufanikiwa.
  11. The secret code of success – Noah ST. John. Kinachowanyima watu mafanikio ni kushindwa kutekeleza (ACTION) matumaini yao halisi, ndoto, na matarajio. Linapokuja suala la mafanikio, akili ya kufikika (conscious mind) si mahali sahihi kuanzia. Sehemu muafaka ya kuanzia ni kwenye subconscious mind maana 90% ya tabia zetu zinatoka huku.
  12. Secrets of the Millionaire Mind – T. Harv Eker. Mafanikio katika jambo lolote yanahitaji kubadili hali ya ndani kwanza kimtazamo ili kubadili matokeo kwa nje kimazingira. Waliofanikiwa kifedha wana picha ya tofauti sana ndani mwao kuhusu fedha ukilinganisha na picha walizo nazo watu maskini na wenye kipato cha kati.
  13. Acres of Diamonds - Russell H. Conwell. Najifunza kupitia simulizi ya jamaa aliyeamua kuuza shamba lake na kusafiri nchi za mbali kwenda kutafuta almasi – bahati mbaya hakuzipata na alifia huko. Huku nyuma, jamaa aliyenunua shamba lake, aligundua lile shamba lilikua limejaa almasi na alichimba akapata nyingi sana. Kwa hiyo, mtu ukiwa na ndoto ya mafanikio, nirahisi kuangalia nje kwa kuamini huko ndiko ndoto yako itatimia, lakini ukweli ni kwamba lazima tuanzie pale tulipo, akilini mwetu, mazingira yetu, na vile tulivyonavyo.
  14. Tatizo si raslimali zilizopotea – Godius Rweyongeza. Huyu Mtanzania kijana ananifundisha kuwa thamani ya mtu inapimwa kwa kile anachotoa si kile unachopokea. Kila mwanadamu angejijua mipaka ya uwezo wake, hakika tusingekuwa hapa leo.
  15. I can, I must, I will – Reginald Abraham Mengi. Kutoka kwa mzee Mengi, napigana Kukataa Hofu ya kushindwa. Hii ni moja ya vitu vikuu vya awali kabisa vinayotufanya watanzania wengi kushindwa kuingia kwenye Biashara. Mengi anasema, tunakosa the “I can” attitude.
  16. Why “A” students work for “C” students and “B” students work for the government – Robert T. Kiyosaki. Nimejifunza kuwa, tunakoelekea watakaoimudu dunia ni wale watakaokuwa na taarifa sahihi, na kuwa tayari kubadirika kadri dunia inavyobadirika na siyo kukinzana na mabadiriko.
  17. Before you quit your job – Robert T. Kiyosaki. Kiyosaki katika kitabu hiki ananifundisha mambo ya kuzingatia kabla ya kuanza safari ya ujasiriamali. Kuna habari ya dhamira, uongozi na timu ya watu. Hizi nguzo tatu, zinabeba ndani mambo matano: mtiririko wa fedha, mawasiliano, mifumo, masuala ya kisheria, na bidhaa. Mtu anapaswa kuwa tayari kwa changamoto zote zijazo. Japo anasema ujasiriamali siyo wa kila mtu, lakini anasisitiza kuwa mtu yeyote anaweza kuwa mjasiriamali.
  18. Increase your financial IQ – Robert T. Kiyosaki. Akili ya fedha si tu kuzalisha fedha zaidi, lakini pia kuzilinda zisipotee, kuzibajeti, kuifanya fedha izae kwa kuwekeza n.k., na kuhakikisha una taarifa sahihi za fedha wakati wote.
  19. Kuna uhusiano kati ya fedha yako na hali yako ya kiroho – Christopher Mwakasege. Fedha ina nguvu kuliko roho kwa mujibu wa maandiko ya biblia kwenye Matayo 6: 21 yanayosema, “Maana pale ilipo hazina yako ndipo utakapokuwa moyo wako”. Mwakasege ananifundisha kuwa, haiwezekani kuapata uhuru wa kiroho vizuri pasipo kwanza kuwa na uhuru wa kifedha. Kwa hiyo, fedha/utajiri ni muhimu sana ili kustawi kiroho.
  20. How to Raise your Own Salary – Napoleon Hill. Hapa najifunza kuwa, watu wenye mafanikio daima wanafanya kazi wanayopenda kufanya. Masaa si kitu kwao. Wanaona furaha katika kufanya kazi yao. Umaskini ni tabia. Mtu yeyote akikubali hali ya umaskini, hali hii ya akili inakuwa tabia. Mtu anakubali umasikini kwa kutokuweka mpango wa kupata utajiri.

No comments:

Post a Comment