Monday, January 14, 2019

SIFA YA WASHINDI KATIKA MAISHA.

“Victory belongs to the most persevering.” - Napoleon Bonaparte
Ushindi unaenda kwa wale ambao ni ving’ang’anizi na wavumilivu.
Huwa tunawaangalia wale waliofanikiwa na kupenda sana kufika walipofika. Lakini sisi wenyewe kuna vitu vingi ambavyo tulishawahi kuanza kwenye maisha yetu, lakini havikutufikisha mbali, kwa sababu tulikosa ung’ang’anizi na uvumilivu.
Sasa chagua kitu kimoja au vichache unavyotaka kwenye maisha yako, kisha weka juhudi zako zote na usikate tamaa mpaka umekipata, na ninakuhakikishia utakipata. Maana washindi wote wameng’ang’ana na kupata walichotaka.

No comments:

Post a Comment