Tuesday, December 25, 2018

WEKA MALENGO YAKO MWEZI DISEMBA KABLA MWAKA HAUJAANZA.

Watu wengi wanakosea kuweka malengo kwa sababu wanayaweka kipindi ambacho siyo sahihi. Wakati wa mwaka mpya, watu wengi huwa wanakuwa na hisia kali za upya wa mwaka na kwa kuwa kila mtu anasema mwaka mpya mambo mapya, basi na wao wanajiunga na msafara huo.
Wengi wanajikuta wanaweka malengo ambayo siyo yao, wanapoona wengine wameweka malengo fulani basi na wao wanaona wanapaswa kuwa na malengo ya aina hiyo. Kitu kinachowapelekea kushindwa sana kwenye maisha yao.

Wakati sahihi wa kuyaweka malengo yako kwa mwaka mpya ni kabla mwaka haujaanza. Hivyo mwezi huu wa disemba, tenga muda na ukae chini ili kuweka malengo yako kwa mwaka unaofuata. Kupitia tafakari ya mwezi ulioisha uliyofanya, kupitia vipaumbele vya mwaka ulivyojiwekea, unaweza kuweka malengo ambayo ni bora sana kwako.

Weka malengo yako ya mwaka mpya mwezi disemba na wakati wengine wanakimbizana na malengo mwanzo wa mwaka, wewe unakuwa upo kwenye utekelezaji.

HERI  YA   X--MASS  NA  MWAKA  MPYA.

No comments:

Post a Comment