Thursday, December 20, 2018

KUWA MTUMWA WA TABIA NZURI KILA SIKU.

Hatua ya kwanza kabisa kwenye kutengeneza mafanikio ni kujijengea tabia nzuri za kila siku na kuwa mtumwa wa tabia hizo. Na wala huhitaji kuanzia mbali sana kujenga tabia nzuri, bali anza na tabia ulizonazo sasa kisha zigeuze kuwa tabia nzuri.

Kwa mfano kama sasa hizi unatumia muda wako mwingi kuangalia tv au kwenye mitandao ya kijamii, jiwekee ukomo kwenye mambo hayo. Mfano jiambie utatenga saa moja pekee kwenye siku yako kwa ajili ya habari, tv na mitandao ya kijamii. Kwa tabia kama hii utaokoa muda wako mwingi ambao kwa sasa unaupoteza.

Kadhalika badili tabia ulizonazo sasa kwenye ulaji, unywaji, muda wa kuamka, muda wa kulala na mengine yote unayofanya kila siku ya maisha yako.
Zoezi la kuchukua; orodhesha tabia zote unazofanya kwenye kila siku yako, kisha angalia zipi ni nzuri kwako na zipi siyo nzuri kwako. Zile nzuri endelea na nazo na zile mbaya zigeuze kuwa nzuri.

No comments:

Post a Comment