Saturday, December 22, 2018

WATU WENGI HUSHINDWA KUYAFIKIA MALENGO YAO ! KWANINI ----------------- ?

Wapo watu ambao wamekuwa wanayaendesha maisha yako kama saa ya mshale ambayo imeharibika. Kwa nje mishale inaweza kuonekana kama inafanya kazi, lakini kwa hakika imesimama.

Wapo watu ambao kila mwanzo wa mwaka huwa wanaweka malengo makubwa, malengo yanayowahamasisha sana na kuwafanya waone wanaweza kufanya makubwa kwenye maisha yao. Lakini siku chache baada ya kuweka malengo hayo, wanajikuta wamesharudi kwenye maisha ya mazoea na kusahau kabisa malengo waliyojiwekea.

Sasa kinachowafanya watu wafanane na saa iliyoharibika ni kwamba mwaka unapoisha na kuanza mwingine, wanaweka tena malengo yale yale na siku chache baadaye wanajikuta wameshayasahau. Hivyo kinachotokea ni mtu kwa miaka mingi anakuwa anarudi kuweka malengo yale yale lakini hachukui hatua wala kuyafikia.

Watu wengi wanaoweka malengo huwa wanashindwa kuyafikia kwa sababu hawavijui vigezo vitano muhimu sana vya kuweka malengo ambayo mtu ataweza kuyafikia.

No comments:

Post a Comment