Thursday, December 20, 2018

ISHI KILA SIKU KWA KIASI.

Kila unachofanya kwenye maisha yako, kinapaswa kuwa kwa kiasi, hupaswi kufanya kwa kiwango kidogo sana wala kufanya kwa kupitiliza.

Kuanzia kwenye maisha binafsi na hata kazi au biashara, fanya kwa kiasi. Usile kupitiliza, usinywe kupitiliza, usiwe na hisia kali kupitiliza na wala usipumzike kupitiliza.

Kuishi kwa kiasi ni tabia muhimu sana ambayo itakuwezesha kufika kwenye mafanikio makubwa. Kwa sababu unapofanya kupita kiasi, unauchosha mwili na unashindwa kufanya yale ambayo ni muhimu.

Zoezi la kufanya; kwa yale unayofanya kila siku kwenye maisha yako, fanya kwa kiasi, jidhibiti wewe mwenyewe usifanye jambo lolote kupitiliza. Usile kupitiliza, kunywa kupitiliza au kupatwa na hisia zilizopitiliza. Kufanya hivyo kutakupeleka kwenye matatizo makubwa.

No comments:

Post a Comment