Thursday, December 20, 2018

KAMILISHA MAJUKUMU YA KILA SIKU.

KAMILISHA majukumu unayojiwekea kila siku. Kila unachopanga kufanya, unapaswa kukifanya kwa muda uliopanga kufanya. Kamwe usiahirishe chochote, usijiambie nitafanya kesho, chochote kinachoweza kufanyika leo kifanye.

Pale wazo la kuahirisha kitu linapoingia kwenye akili yako, mara moja jiambie NITAFANYA SASA, rudia maneno hayo mara nyingi na utasahau kuhusu kuahirisha na kuweza kuchukua hatua mara moja.

Zoezi la kufanya; kila unachoorodhesha kufanya kwenye siku yako kifanye, usiwe mtu wa kuahirisha mambo. Wazo la kuahirisha linapokujia, jiambie NITAFANYA SASA, kisha fanya.

No comments:

Post a Comment