Thursday, December 20, 2018

WEKA AKIBA SEHEMU YA KUMI YA KIPATO CHAKO.

Kwenye kila kipato unachoingiza, asilimia kumi ya kipato hicho hupaswi kuitumia kwa shughuli nyingine yoyote, bali unapaswa kujilipa wewe mwenyewe. Hichi ni kipato ambacho unakiweka pembeni maalumu kwa ajili ya uwekezaji ambao utakulipa zaidi baadaye.
Unapopata fedha, kabla hujaanza kulipa bili mbalimbali unazodaiwa au kununua vitu unavyohitaji, jilipe wewe mwenyewe kwanza. Hii ni tabia moja rahisi ambayo imewawezesha wengi kufikia utajiri mkubwa, bila ya kujali kiasi cha kipato walichonacho. Unapaswa kujilipa kwanza kabla hujafanya matumizi, kwa sababu ukisema utumie halafu itakayobaki ndiyo ujilipe, hutabakiwa na kitu.
Zoezi la kufanya; kwenye kila kipato unachoingiza, kabla hujaanza kupangilia unakitumiaje, ondoa kwanza asilimia kumi ya kipato hicho na weka pembeni, weka mahali ambapo hutakitumia hata iweje. Kipato hicho ni kwa ajili ya uwekezaji, ndiyo kitakachokufanyia wewe kazi.

No comments:

Post a Comment