Tuesday, December 25, 2018

KUWA MAKINI NA MSIMU WA SIKUKUU USIKUACHE MWEUPE PEPEEE !!

Mwezi disemba ni mwezi ambao huwa kuna sikukuu nyingi, ni mwezi ambao wengi wana mategemeo makubwa ya kupumzika na kusherekea. Lakini unapaswa kuwa makini sana na kipindi cha sikukuu kwa sababu wengi hujisahau na kuuanza mwaka wakiwa kwenye madeni makubwa.

Hakikisha unajiwekea bajeti ya matumizi yako kwenye msimu wa sikukuu, na usizidishe kabisa bajeti hiyo. Hakikisha unaamua mapema kabisa ni vitu gani utagharamia kwenye msimu huo wa sikukuu na vipi utaachana navyo.

Na kama kuna sherehe ambazo hazina ulazima, zisikuumize kichwa, achana nazo. Hakuna utakachokikosa kwa kuachana na baadhi ya sherehe na mapumziko. Pia kama utaanza kufanyia kazi malengo yako mapema, utakuwa bize kupiga hatua na sikukuu hazitakuwa na madhara kwako.

HERI  YA  X--MASS  NA  MWAKA  MPYA.

No comments:

Post a Comment