Thursday, December 20, 2018

KUWA NA FIKRA ZA KITAJIRI KILA SIKU.

Kuna fikra za kitajiri na fikra za kimasikini. Fikra za kitajiri ni fikra chanya, za hamasa na matumaini makubwa. Fikra za kimasikini ni fikra hasi, za kukata tamaa na kushindwa.
Ili uweze kufanikiwa unapaswa kuwa na fikra za kitajiri kila siku, unapaswa kuwa na kauli chanya ambazo unajiambia kila siku, kauli ambazo zinakupa hamasa na kukusukuma kusonga mbele zaidi. Jijengee taswira ya kile unachotaka kwenye maisha yako na mara kwa mara jione umeshapata kitu hicho. Kwa kufanya hivi unaipa akili yako kazi ya kuhakikisha unapata unachotaka.
Zoezi la kufanya leo; dhibiti fikra zako ziwe chanya na za kitajiri kila siku. Fikiria yale ambayo yanakufikisha kwenye kile unachotaka. Jione tayari umeshafika pale unapotaka na weka picha hiyo kwenye akili yako mara zote. Hili litakufanya uvutie mazingira yatakayokuwezesha kupata unachotaka.

No comments:

Post a Comment