Tuesday, August 13, 2019

ELIMU YA DARASANI INAPOKWAMA.

“In the new world of sales, being able to ask the right questions is more valuable than producing the right answers. Unfortunately, our schools often have the opposite emphasis. They teach us how to answer, but not how to ask.” ― Daniel H. Pink
Kwenye ulimwengu mpya wa mauzo, kuuliza maswali sahihi ni bora kuliko kuwa na majibu sahihi. Kwa sababu tayari mteja anajua mengi zaidi, jukumu lako kama muuzaji ni kuuliza maswali yatakayokupa wewe fursa ya kumjua mteja zaidi.

Lakini kwa bahati mbaya sana, elimu ya darasani iko kinyume na hili. Miaka yote ambayo tumekaa shuleni tumekuwa tunafundishwa jinsi ya kujibu maswali ili kufaulu mtihani. Hivyo unakuwa vizuri sana kwenye kujibu maswali, lakini unapofika mtaani unakuta tayari kila mtu ana majibu. Hivyo elimu ya darasani inakwama hapo.

Ili kupiga hatua kwenye kitu chochote unachofanya kwenye maisha yako, jifunze jinsi ya kuuliza maswali sahihi, maswali ambayo yatakupa nafasi ya kumjua mtu zaidi na mahitaji yake, ili uweze kumhudumia zaidi.

Kadiri unavyoweza kuuliza maswali sahihi na kusikiliza kwa makini majibu yanayotolewa, ndivyo unavyoweza kujifunza na kujua hatua sahihi za kuchukua.

No comments:

Post a Comment