Sunday, August 18, 2019

CHAGUA SHUJAA WA MAISHA YAKO.

Wastoa wamekuwa wanaelewa umuhimu wa kuwa na mashujaa, watu ambao tunayapima maisha yetu kupitia wao. Lakini hili ni eneo ambalo limekuwa na changamoto kubwa sana zama hizi, kwa sababu kumekuwa na mashujaa wengi feki. Siku hizi watu wanaoweza kutengeneza umaarufu rahisi kupitia mitandao ya kijamii, sanaa, michezo au siasa ndiyo wanaonekana mashujaa kwa wengi. Na wengi wanawafuata watu hao, lakini hakuna wanachojifunza kwa sababu mwisho wa siku umaarufu wa watu hao huanguka, kwa sababu haujajengwa kwenye misingi sahihi.
Ni muhimu uchague mashujaa sahihi wa maisha yako, kutokana na misingi wanayoiishi au waliyoiishi ambayo unaweza kujijengea kwenye maisha yako na ukaweza kupiga hatua pia. Kadiri unavyojifunza falsafa hii na kujifunza wengine walioiishi falsafa hii, utavutiwa na maisha ya baadhi ya wanafalsafa na kuwachagua kuwa mashujaa wako.

No comments:

Post a Comment