Friday, October 12, 2018

UTOAJI WA FEDHA KWA WENGINE BILA KUTEGEMEA KUPATA CHOCHOTE NI MUHIMU SANA.

Kiasi cha fedha unachotoa kwa wengine bila ya kutegemea kupata chochote ni kiwango kingine muhimu sana cha kupima afya yako kifedha na kujua hatua ulizopiga. Kwa kadiri unavyotoa zaidi ndivyo unavyoonesha kwamba unaitumia fedha na siyo fedha inakutumia wewe.

Unahitaji kuwa na utaratibu wa kutoa fedha kuwasaidia wengine bila ya kutegemea kulipwa fedha hizo. Kwa sababu tunatoshelezwa zaidi na utoaji kuliko upokeaji.

Pia unapotoa fedha kwa wengine, unatengeneza pengo ambalo itabidi lizibwe, hivyo unakuwa umejiweka kwenye nafasi ya kuongeza kipato chako zaidi.

No comments:

Post a Comment