Friday, October 12, 2018

KILA MTU ANA NAMBA NA VIWANGO VYAKE KIFEDHA. HATUWEZI KULINGANA.

Linapokuja swala la fedha, kila mtu ana namba na viwango vyake. Kwa sababu tunatofautiana ndoto, kazi/biashara, kipato, mitindo ya maisha na hata mazingira, matokeo yetu ya kifedha hayawezi kulingana.

Hivyo kujipima hatua ulizopiga kifedha kwa kuwatumia wengine ni kujiumiza na hata kujirudisha nyuma, kwa sababu kuna namba nyingi ambazo utakuwa huzijui kuhusu wengine. Kwa mfano unaweza kumwona mtu kwa nje anaonekana kuwa na vitu vinavyoashiria ana fedha nyingi, lakini kumbe vitu vyote hivyo amepata kwa mkopo ambao ataulipa maisha yake yote.
Pia unaweza kumwona mtu ukafikiri hayupo vizuri kifedha kwa mwonekano wake wa nje, kumbe anafanya uwekezaji ambao baadaye utamwezesha kufikia uhuru wa kifedha.

Kwa kuwa ni vigumu kupima hatua ulizopiga kifedha kwa kuwatumia watu wengine, unahitaji kujitumia wewe mwenyewe.

No comments:

Post a Comment