Sunday, October 7, 2018

ISHI KULINGANA NA MISINGI YA ASILI

Huwa tunayaona maisha yetu ni magumu na tuna mengi ya kukabiliana nayo, lakini hebu fikiria jinsi ulimwengu unavyojiendesha. Fikiria jinsi ambavyo sayari yetu ya dunia inalizunguka jua mwaka mzima, na kutupatia majira ya mwaka. Fikiria jinsi sayari hii inajizungusha kwenye mhimili wake kila siku na kutupatia usiku na mchana. Asili imeyapangilia mambo yake ambayo yanajiendesha vizuri.

Sisi pia tunapaswa kuishi kwa msingi wa asili, kujua kile ambacho tunapaswa kufanya, kujipanga kukifanya na kukifanya kwa ubora na msimamo kama ambavyo asili inafanya mambo yake. Kwa kuishi kulingana na asili, hata matatizo yetu yanayotusumbua yanaonekana ni madogo sana ukilinganisha na jinsi ulimwengu mzima unavyojiendesha.

 Kazi za Mungu ndiyo zinatupa sisi riziki, na kazi za asili hazitofautiani na asili yenyewe. Kila kitu kinatokana na asili. Kila kitu ambacho ni muhimu na kinachohitajika na ulimwengu mzima kinatokana na asili. Kila kinachotokana na asili na kila kinachoitunza asili ni kizuri kwa kila sehemu ya asili. Mabadiliko ya kipengele chochote kwenye asili, ndiyo yanaufanya ulimwengu kuwa kama ulivyo.

No comments:

Post a Comment