Monday, October 8, 2018

USISINGIZIE HAUNA MUDA WA KUTOSHA KUFANYA YALE MUHIMU.

Moja ya kisingizio cha watu wengi kwenye kushindwa kufanya yale wanayotaka kufanya kimekua ni muda. Muda unaonekana kuwa mfupi sana na mambo ya kufanya yakiwa mengi. Hivyo tumekuwa tunatamani kama masaa ya siku yangeongezwa ili tuweze kufanya zaidi.
Lakini ukweli ni kwamba, masaa ya siku hayataongezeka, ni yale yale 24. Na wale wanaofanikiwa sawa sawa na wanaoshindwa, wana masaa hayo hayo kwa siku. Sasa kwa nini wachache wafanikiwe kwenye muda huo, wakati wengi wanashindwa na kuona hawana muda?
Seneca analo jibu zuri sana kwetu kuhusu muda;
Life is long enough, and a sufficiently generous amount has been given to us for the highest achievements if it were all well invested. But when it is wasted in heedless luxury and spent on no good activity, we are forced at last by death’s final constraint to realize that it has passed away before we knew it was passing. So it is: we are not given a short life but we make it short, and we are not ill-supplied but wasteful of it. Just as when ample and princely wealth falls to a bad owner it is squandered in a moment, but wealth however modest, if entrusted to a good custodian, increases with use, so our lifetime extends amply if you manage it properly. – Seneca, On The Shortness Of Life.
Maisha ni marefu vya kutosha na muda wa kutosha tumepewa kwa kufikia yale makubwa kama tutauwekeza muda huo vizuri. Lakini tunapopoteza muda huo kwa anasa zisizo na maana na kushindwa kufanya yale mazuri, tunakuja kustuka tumepoteza muda na maisha yetu pale tunapofikia kifo. Hivyo basi, siyo kwamba tuna maisha mafupi, bali tunayafanya kuwa mafupi, siyo kwamba muda ni mdogo, bali tunao mwingi mpaka tunaupoteza. Kama ambavyo utajiri ukiwa kwenye mikono ya mtu asiye makini unapotea na ukiwa kwenye mikono ya mtu makini unakua, ndivyo maisha yetu yalivyo, yanakua kama yataendeshwa vizuri.

No comments:

Post a Comment