Sunday, October 7, 2018

FANYA YALIYO NDANI YA UWEZO WAKO, USISUMBUKE NA YALIYO NJE YA UWEZO WAKO

Sisi binadamu huwa tunasumbuka na mambo mengi sana, lakini tukianza kuyaangalia mambo hayo, mengi tunajisumbua nayo bure, kwa sababu yapo nje ya uwezo wetu, hakuna chochote tunachoweza kufanya tukayabadili au kuyaathiri.
Mambo yote yanayotokea kwenye maisha yetu tunaweza kuyagawa kwenye makundi mawili, yaliyo ndani ya uwezo wetu, haya ni yale ambayo tunaweza kuyaathiri, tunaweza kuyafanya kuwa bora zaidi. Na kuna yale ambayo yapo nje ya uwezo wetu, ambapo hatuna cha kufanya.

 Baadhi ya vitu vipo ndani ya uwezo wetu na vingine vipo nje ya uwezo wetu. Vilivyo ndani ya uwezo wetu ni maoni yetu, fikra zetu, maamuzi yetu na matendo yetu, kwa kifupi yale yote ambayo sisi tunayafanya. Vitu vilivyo nje ya uwezo wetu ni miili yetu, mali zetu, sifa zetu na nafasi nyingine tunazopewa, kwa kifupi chochote ambacho hatufanyi sisi moja kwa moja, kipo nje ya uwezo wetu. Vitu vilivyo ndani ya uwezo wetu ni bure, huru na visivyo na ukomo, vilivyo nje ya uwezo wetu ni dhaifu, visivyo huru, vyenye ukomo na visivyo vyetu.

Kwa vyovyote vile, hupaswi kusumbuliwa na chochote, kwa sababu kama kitu kipo ndani ya uwezo wako basi unahitaji kuchukua hatua, na kama kipo ndani ya uwezo wako huna hatua ya kuchukua hivyo kubaliana nacho kama kilivyo au kipuuze.

No comments:

Post a Comment