Monday, October 8, 2018

TENGENEZA NJIA , USIFUATE NJIA

”Do not go where the path may lead, go instead where there is no path and leave a trail.” – Ralph Waldo Emerson

Watu wengi wamekuwa wanashindwa kwenye maisha kwa sababu hawathubutu kufanya vitu vipya, badala yake wanaangalia kile ambacho tayari kimeshafanya na wao wanafanya. Hii ni kufuata njia, sasa unapochagua kufuata njia fulani, jua utafika kule ambapo njia hiyo imeelekea. Kama utafanya kile ambacho wengine wanafanya, utapata matokeo ambayo wanayapata.

Njia pekee ya kufanikiwa zaidi, ni kufanya mambo mapya, kufanya yale ambayo hakuna mwingine anayefanya, kutengeneza njia mpya, pale ambapo hakuna njia. Hili linatisha, kwa sababu unakuwa huna uhakika, nafasi ya kushindwa ni kubwa, lakini pia nafasi ya kufanikiwa ni kubwa zaidi.
Kwenye chochote unachochagua kufanya, acha kuangalia wengine wanafanya nini ili uige, badala yake angalia kipi muhimu kinachopaswa kufanya kisha kifanye kwa njia ambayo ni sahihi kwako kufanya na kwa wale unaowahudumia. Kwa namna hii utatengeneza njia mpya na wewe kama kiongozi wa njia hiyo utanufaika zaidi.
Rafiki, sindano za leo zimekuwa ndefu na kali, lakini kama utazifanyia kazi, hutabaki hapo ulipo. Sina kingine cha kuongeza zaidi ya kukukumbusha kanuni yetu muhimu ambayo ni MAARIFA SAHIHI + KUCHUKUA HATUA KUBWA = MAFANIKIO MAKUBWA. Maarifa ni hayo, kazi kwako kuchukua hatua ili ufanikiwe.

No comments:

Post a Comment