Sunday, October 7, 2018

JIJENGEE TABIA NJEMA KATIKA MAISHA YAKO

Tabia njema ni moja ya misingi muhimu sana kwenye falsafa ya ustoa. Kadiri unavyojijengea na kuishi kwa tabia njema, ndivyo unavyojitengenezea maisha bora na yenye furaha wakati wote. Tabia njema ndiyo zao la furaha. Kwenye ustoa, tabia njema ni pale unapoishi na kusimamia yale yenye maana kwako na kwa wengine, na kuachana na yale yasiyo na maana.
Kwenye ustoa kuna tabia njema kuu nne;
HEKIMA; Ubora katika kufikiri na kufanya maamuzi.
UJASIRI; Uwezo wa kukabiliana na hatari kwa usahihi.
HAKI; Ubora katika mahusiano yetu na wengine.
KIASI; Uwezo wa kudhibiti hisia na tamaa.
Marcus ana haya ya kutuambia kuhusu tabia njema;

If you can find anything in human life better than justice, truthfulness, selfcontrol, courage […] turn to it with all your heart and enjoy the supreme good that you have found […] but if you find all other things to be trivial and valueless in comparison with virtue, give no room to anything else, since, once you turn towards that and divert from your proper path, you will no longer be able without inner conflict to give the highest honour to what is properly good. It is not right to set up as a rival to the rational and social good anything alien to its nature, such as the praise of the many, or positions of power, wealth, or enjoyment of pleasures. – Marcus Aurelius, Meditations, 3.6
Kama unaweza kupata kitu bora kwenye maisha ya mtu zaidi ya haki, ukweli, kujidhibiti na ujasiri, kishikilie sana kitu hicho. Lakini kama utakuta vitu vingine ni visivyo na maana ukilinganisha na tabia njema, usitoe nafasi kwa kitu kingine bali tabia hizo njema. Kwa sababu utakapoacha njia yako sahihi hutaweza tena kuzingatia yale ambayo ni mazuri kwako. Siyo sahihi kuleta upinzani kati ya fikra sahihi na vitu vya nje kama sifa kutoka kwa wengine, nafasi za madaraka, utajiri na kufurahia raha.

No comments:

Post a Comment