Monday, October 8, 2018

USIRUHUSU HISIA ZAKO ZIKUTAWALE , THIBITI HISIA ZAKO, USITAFSIRI TUKIO.

Moja ya changamoto kubwa zinazowapelekea wengi kushindwa kwenye maisha ni kuendeshwa na hisia badala ya wao kuendesha hisia zao. Wote tunajua kwamba pale tunaporuhusu hisia zitutawale, tunakuwa tumeondoa kabisa uwezo wetu wa kufikiri. Kwa sababu hisia kali na fikra haviwezi kukaa pamoja.

Kupitia falsafa ya ustoa, tunajifunza kwamba hisia ni kitu ambacho tunakitengeneza sisi wenyewe na hakuna anayetupa, hivyo tunaweza kuchagua kutoruhusu hisia zitawale maamuzi yetu.
Epictetus ana maneno mazuri ya kutuambia kuhusu hisia;
It isn’t the things themselves that disturb people, but the judgements that they form about them. Death, for instance, is nothing terrible, or else it would have seemed so to Socrates too; no, it is in the judgement that death is terrible that the terror lies. Accordingly, whenever we are impeded, disturbed or distressed, we should never blame anyone else but only ourselves, that is, our judgements. It is an act of a poorly educated person to blame others when things are going badly for him; one who has taken the first step towards being properly educated blames himself, while one who is fully educated blames neither anyone else nor himself. – Epictetus, Handbook, 5
Kinachotusumbua siyo kile kinachotokea, bali tafsiri yetu kwa kile kinachotokea. Kwa mfano kifo, siyo kitu cha kutisha, kama ingekuwa hivyo wanafalsafa kama Socrates wangekiogopa. Ni tafsiri yetu kwamba kifo ni kitu kibaya ndiyo inatusumbua. Hivyo hivyo, tunapokuwa tumekwazika, tumesumbuka au kupata msongo, hatupaswi kumlaumu mtu yeyote bali sisi wenyewe, kwa sababu hivyo vinatokana na tafsiri zetu wenyewe. Kwa asiyekuwa na elimu, huwalaumu wengine pale mambo mabaya yanapomtokea, anayeanza kujifunza hujilaumu mwenyewe wakati yule aliyeelimika hamlaumu yeyote wala hajilaumu yeye mwenyewe.

No comments:

Post a Comment