Sunday, October 7, 2018

JENGA MAHUSIANO BORA KATIKA MAISHA YAKO

Sisi binadamu ni viumbe wa kijamii, hatuwezi kuishi kwa kujitegemea wenyewe kwa kila kitu. Hivyo mahusiano yetu na wengine ni moja ya vitu muhimu sana kwetu ili kuweza kuwa na maisha bora.
Falsafa ya ustoa inatufundisha jinsi ya kutengeneza mahusiano bora na wale wanaotuzunguka kwa kuimarisha mahusiano yetu na ushirikiano kwenye mambo mbalimbali.
Njia bora ya kuimarisha mahusiano na ushirikiano ni kuangalia tabia nzuri zilizopo ndani ya wengine badala ya kuangalia mabaya pekee. Pia kuangalia namna ya kushirikiana na siyo kupingana.
Marcus ana maneno mazuri ya kutuambia kuhusu mahusiano;
Say to yourself first thing in the morning: I shall meet with people who are meddling, ungrateful, violent, treacherous, envious, and unsociable. They are subject to these faults because of their ignorance of what is good and bad. But I have recognised the nature of the good and seen that it is the right, and the nature of the bad and seen that it is the wrong, and the nature of the wrongdoer himself, and seen that he is related to me, not because he has the same blood or seed, but because he shares in the same mind and portion of divinity. So I cannot be harmed by any of them, as no one will involve me in what is wrong. Nor can I be angry with my relative or hate him. We were born for cooperation, like feet, like hands, like eyelids, like the rows of upper and lower teeth. So to work against each other is contrary to nature; and resentment and rejection count as working against someone. – Marcus Aurelius, Meditations, 2.1
Jiambie hili kitu cha kwanza asubuhi: Leo nakwenda kukutana na watu ambao ni waovu, wasio na shukrani, wenye fujo, wasaliti, wenye wivu na wasiojali. Watu hao wako hivyo kwa sababu hawajui kipi kizuri na kipi kibaya. Lakini mimi natambua asili ya uzuri na nimeona kipi sahihi na asili ya ubaya na kuona kipi kisicho sahihi na asili ya wanaofanya ubaya na kuona wana uhusiano na mimi, kwa sababu wana damu sawa na yangu na tunashirikiana mawazo yetu. Siwezi kuumizwa na yeyote kwa sababu hakuna anayeweza kunihusisha kwenye ubaya wake. Pia siwezi kuwa na hasira au kumchukia ndugu yangu. Sote tumezaliwa kwa ushirikiano, kama miguu, mikono, kope za macho, meno ya juu na ya chini. Hivyo kufanya kazi kwa kupingana ni kinyume na asili na chuki na kukataana ni kufanya kazi kinyume na wengine.

No comments:

Post a Comment