Saturday, June 22, 2019

KWANINI UTAKE KUUZA BIASHARA YAKO ?

"John  Warrillow "  katika  Kitabu   Chake  " BUILT  TO  SELL " anatuambia zipo sababu mbalimbali za wewe kutaka kuuza biashara unayokuwa umeianzisha.
  1. Biashara yako inaweza kuwa ndiyo chanzo chako cha mafao unapostaafu, hivyo kuweza kuiuza kunakupa kiasi kikubwa cha fedha cha kustaafu bila ya shida.
  2. Unaweza kuwa unataka kuanzisha biashara nyingine. Wajasiriamali huwa wanachoka kitu haraka, hivyo ukianzisha biashara na kuona tayari umeichoka na kuna biashara nyingine unapenda kuingia, unaweza kuuza ile uliyonayo sasa.
  3. Unaweza kuwa na uhitaji mkubwa wa fedha kutatua matatizo mbalimbali yanayokukumba. Biashara yako inaweza kuwa kama akiba au uwekezaji wako, ambao unaweza kuuza pale unapokuwa na uhitaji mkubwa wa fedha kutatua changamoto mbalimbali za maisha yako.
  4. Unaweza kuwa unahitaji kupata muda zaidi kwa ajili yako na familia yako. Pale unapoona biashara yako inachukua muda kuliko unavyoweza kuipa, unaweza kuchagua kuiuza.
  5. Unaweza kuwa unahitaji kulala vizuri usiku bila ya wasiwasi, kwa sababu unapokuwa mjasiriamali, unakuwa na usiku mwingi ambao hulali, unafikiria biashara itakuaje, ushindani utaushindaje, mishahara utalipaje, mikopo unarejeshaje na mengine mengi ambayo yatakunyima usingizi. Lakini unapojua kwamba unaweza kuiuza biashara hiyo muda wowote, unakuwa na utulivu mkubwa wa akili.

No comments:

Post a Comment