Saturday, June 22, 2019

KWANINI BIASHARA NYINGI HAZIFAI KUUZA ?

Biashara nyingi hazifai kuuza kwa sababu zinaendeshwa kwa vurugu. Kwa nje biashara inaweza kuonekana inakwenda vizuri, lakini kwa ndani mambo ni vurugu. Hakuna mpangilio wowote wala mfumo ambao unafuatwa. Kila kitu kinafanywa kwa namna ambavyo mtu anajisikia kufanya. Hakuna viwango vyovyote vinavyofanyiwa kazi.
Wateja wanaokuja kupata huduma kwenye biashara, hawaji kwa sababu ya biashara, bali wanakuja kwa sababu ya mtu. Na wengine wanasema wazi kwamba wanataka kuhudumiwa na fulani tu.
Wafanyabiashara wengi hufurahia pale wateja wanapotaka wahudumiwe na wao tu, wakiona ni wateja wanawaamini na kuwakubali sana. Lakini wasijue kama hicho ndiyo kifungo chao.
Huwezi kuuza biashara ambayo haiendeshwi kwa mfumo na kila kitu kinamtegemea mmiliki wa biashara hiyo.
Na biashara ya aina hii inakuwa mzigo kwa mmiliki na kumnyima uhuru.
Karibu tujifunze jinsi ya kutengeneza biashara inayokupa uhuru na unayoweza kuiuza muda wowote na hili litakuwezesha kuwa na biashara bora na isiyokutegemea kwa kila kitu. Na hata kama hutaki kuuza biashara yako, kitendo cha biashara kuweza kujiendesha yenyewe bila ya wewe kuwepo, utakuwa ushindi mkubwa sana kwako.

No comments:

Post a Comment