Thursday, June 20, 2019

ISHI MAISHA YAKO, USIWE MTU WA CHUKI, SAMBAZA UPENDO

Kuna  watu wenye chuki, ambao kwa sababu tusizozijua, wanaamua kutuchukia, kwa jinsi tulivyo au kwa kile tunachofanya.
 
Wengi wamekuwa wanashangaa inakuwaje watu wawachukie, na hili ni kupoteza muda. Watu wenye chuki huwa wanachukia, na huna lolote unaloweza kufanya kuwafanya wasikuchukie.
 
Watu wenye chuki hawabadiliki na kuacha kuwa na chuki kwa sababu wewe umefanya kitu fulani, bali wataendelea kupata sababu za kuwa na chuki zaidi.
 
Hivyo badala ya kuishi maisha ya kutaka kuwaridhisha wengine, hasa wale wenye chuki, ishi maisha yako, fanya kile ambacho ni muhimu kwako na simamia kile unachoamini.
 
Wenye chuki watachukia iwe unaishi maisha yako au unafanya wanachotaka wao.
 
Usiyumbishwe na wenye chuki, chagua kuyaishi maisha yako.
 
Na kwa upande wa pili, usiwe mtu wa chuki, sambaza upendo.

No comments:

Post a Comment