Sunday, September 16, 2018

WEKA MKAZO KATIKA THAMANI YA MAISHA YA MTEJA , GHARAMA YA KUMPATA MTEJA NA KIWANGO CHA WATEJA WANAOPATIKANA KWENYE BIASHARA YAKO UTAFANIKWA SANA.

Ili biashara yako ifanikiwe, inahitaji kuweka mkazo kwenye maeneo haya matatu muhimu sana.

(1). THAMANI YA MAISHA YA MTEJA. Wafanyabiashara wengi huwa wanamwangalia mteja kwa wakati ule anaokuja kununua tu. Huwa hawaangalii thamani yake ya maisha. Kwa mfano kama mteja akija kununua kwako mara moja, unapata faida ya shilingi elfu moja, ni rahisi kuona elfu moja inakuja. Lakini chukua mfano kwamba mteja huyo ananunua kila wiki, na anaweza kununua kwako kwa miaka mitano ijayo. Hii ina maana kwa mwaka, anakuingizia faida ya 1000 x 52(idadi ya wiki za mwaka) ambayo ni tsh 52,000/= na kwa miaka mitano; 5 x 52,000/= ambayo ni sawa na 260,000/=. Thamani ya maisha ya mteja wako huyo ni shilingi laki mbili na elfu sitini, na siyo ile elfu moja unayoiona anapokuja. Je kwa kujua hilo hutaongeza umakini zaidi kwa mteja huyu ili aendelee kuwa na wewe kwa miaka hiyo mitano na hata zaidi?

(2).GHARAMA YA KUMPATA MTEJA. Hapa ndipo gharama za kununua wateja wa biashara yako zinapoingia. Kabla hujachukua hatua yoyote ya kuongeza wateja zaidi kwenye biashara yako, lazima ujiulize gharama unayotumia inaleta wateja wangapi na kama gharama hizo zinarudi kupitia mauzo. Upo usemi kwenye utangazaji wa biashara kwamba nusu ya bajeti ya matangazo huwa inapotea, ila mtu hawezi kujua ni nusu ipi. Hii ina maana kwamba, gharama nyingi watu wanazotumia kutangaza biashara zao zinapotea, hazirudi kabisa kwenye biashara. Lazima ujue gharama zako na zinarudije.

(3). KIWANGO CHA WATEJA WAPYA WANAOPATIKANA. Unapotangaza biashara yako, watu wengi wanajua kuhusu uwepo wako. Lakini watu kujua kuhusu biashara yako hakukunufaishi chochote. Ni mpaka pale watu hao watakapochukua hatua ya kununua ndiyo biashara inanufaika, kama gharama zimepigwa vizuri. Hivyo eneo la kuweka mkazo ni kuongeza kiwango cha wanaojua biashara kuwa wateja wa biashara hiyo. kadiri watu wengi wanaofikiwa na tangazo wanakua wateja, ndivyo gharama za kupata wateja zinakuwa ndogo na faida inakuwa kubwa baadaye.


 Na  Mwl  Japhet  Masatu , Dar  es  salaam , Tanzania,  Afrika Ya  Mashariki ---Mwl  wa  Maisha Na  Mafanikio, Mshauri, Public Speaker(MC), Mwandishi, Mjasiriamali /
Tuwasiliane kwa :+ 255 755 400 128 / + 255 716 924136(WhatsApp ).  EMAIL: japhetmasatu@gmail.com

No comments:

Post a Comment