Sunday, September 16, 2018

JE, UMEAJIRIWA ? AU WEWE NI MFANYABIASHARA ? ONGEZA KIPATO CHAKO KILA MWEZI KWA KUFANYA HIKI.

Rafiki, kwenye eneo la fedha, ukuaji unapimwa kwa ongezeko lako la kipato. Na ongezeko siyo la mwaka, bali la mwezi. Kila mwezi, inabidi kipato chako kiwe kinaongezeka.
Kama kipato chako kinabaki pale pale kila mwezi, kama ilivyo kwa waajiriwa na hata wafanyabiashara wengi, siyo kwamba unabaki pale pale, bali unarudi nyuma kwa upande wa kipato.
Kwa sababu kila siku gharama za maisha zinaongezeka, hivyo kipato kisipoongezeka, unazidi kurudi nyuma.
Njia pekee ya kuongeza kipato chako kila mwezi ni kutoa thamani zaidi kwa wengine. Kama upo kwenye biashara hilo ni rahisi, uzia wateja wengi zaidi kila mwezi, hata kupata mteja mmoja wa ziada kila mwezi ni hatua nzuri. Wauzie wateja ulionao zaidi kila mwezi, na pia ongeza bidhaa na huduma ambazo wateja wako wanahitaji pia.
Kwa walioajiriwa, pia unaweza kuongeza thamani zaidi kwenye kazi yako au nje ya kazi yako na ukaongeza kipato chako. Kama una utaalamu fulani, tumia utaalamu huo nje ya kazi yako kwa kutoa huduma za utaalamu huo. Unaweza kutoa huduma za ushauri kulingana na utaalamu ulionao na watu wakalipia msaada ambao unakuwa umewapatia.
Chochote unachofanya, hakikisha kila mwezi kipato chako kinaongezeka zaidi. Na hivyo ni muhimu kila mwezi ukapiga hesabu za kujua kipato chako ni kiasi gani.


 Na  Mwl  Japhet  Masatu , Dar  es  salaam , Tanzania,  Afrika Ya  Mashariki ---Mwl  wa  Maisha Na  Mafanikio, Mshauri, Public Speaker(MC), Mwandishi, Mjasiriamali /
Tuwasiliane kwa :+ 255 755 400 128 / + 255 716 924136(WhatsApp ).  EMAIL: japhetmasatu@gmail.com

No comments:

Post a Comment