Saturday, September 15, 2018

UKIFANYA KWA MSUKUMO WA NDANI , UTAPATA PESA SANA.

Kwa chochote ambacho unafanya kwenye maisha yako, kuna misukumo au hamasa za aina mbili.
(2):-
         Aina ya kwanza ni msukumo au hamasa inayotoka ndani yako. Hapa ni pale unapofanya kitu kwa sababu umechagua kufanya, kwa sababu unajua ni kitu muhimu kwako kufanya na kwa sababu unajua kuna thamani unaongeza kwenye maisha ya wengine.

        Aina ya pili ni msukumo au hamasa inayotoka nje. Hapa ni pale unapofanya kitu ili kuonekana unafanya, au kwa sababu wengine wanafanya, au kwa sababu watu wanakutegemea ufanye hivyo. Pia unaweza kuwa unafanya ili upate kitu fulani unachotaka.(BENDERA  FUATA  UPEPO ).

(1) .MSUKUMO  AU   HAMASA KUTOKA  NDANI

Msukumo wa ndani yako ndiyo wenye nguvu sana, kwa sababu utafanya licha ya kinachoendelea nje yako. Lakini msukumo wa nje hauna nguvu kubwa, kwa sababu mazingira ya nje yakibadilika, basi na msukumo unabadilika.
Sasa kama unataka kupata fedha zaidi, tafiti zinaonesha kwa kutumia msukumo wa ndani unaweza kutengeneza fedha mara tatu zaidi ya unavyotumia msukumo wa nje.
Pale unapofanya kitu kwa sababu umechagua kufanya, kwa sababu unataka kuwasaidia wenye uhitaji au unataka kutoa mchango wako, utatengeneza kipato kikubwa kuliko pale unapofanya ili tu upate fedha ya kulipa gharama za maisha yako.
 
Unapofanya kitu kwa sababu tu unataka fedha, unapata fedha kidogo, kuliko kama utafanya kitu hicho hicho kwa msukumo kutoka ndani yako.
Na pale unapofanya kitu kwa msukumo wa ndani, haimaanishi kwamba hujali fedha, unajali sana, ila msukumo wa wewe kufanya ni mkubwa kuliko fedha, hivyo unakuwa umejiweka juu ya fedha, kitu ambacho kinakuwezesha kupata fedha kama unavyotaka.



(2).MSUKUMO  AU   HAMASA  KUTOKA  NJE

Lakini unapofanya kwa ajili ya fedha pekee, utapata fedha, lakini utakuwa umeweka fedha juu yako, hivyo unakuwa umejiwekea ukomo wewe mwenyewe, ukishafika kiwango fulani cha fedha utaacha kufanya kwa sababu hamasa yako ilikuwa fedha pekee.

Kuwa na msukumo wa ndani kwenye kila unachofanya, penda fedha na ihitaji, lakini isiwe msukumo pekee wa wewe kufanya kitu. Fanya unachofanya kwa msukumo wa ndani na utaweza kupata fedha kadiri utakavyo, na hutakuwa na ukomo wowote kwenye kipato unachoweza kutengeneza.


 Na  Mwl  Japhet  Masatu , Dar  es  salaam , Tanzania,  Afrika Ya  Mashariki ---Mwl  wa  Maisha Na  Mafanikio, Mshauri, Public Speaker, MC,Mwandishi, Mjasiriamali /
Tuwasiliane kwa :+ 255 755 400 128 / + 255 716 924136(WhatsApp ).  EMAIL: japhetmasatu@gmail.com


No comments:

Post a Comment