Sunday, September 16, 2018

USITAFUTE MCHAWI WA MAISHA YAKO , MCHAWI NI WEWE MWENYEWE !!

‘Be miserable. Or motivate yourself. Whatever has to be done, it’s always
your choice.’ – Wayne Dyer
kama unajisikia vibaya, hilo ni tatizo lako ninafsi. Wala usitafute mtu wa kumlaumu, hakuna anayeharibu siku yako ila wewe mwenyewe. Hakuna anayeharibu maisha yako ila wewe mwenyewe. Wewe ndiye unayechagua ufikirie nini, usikilize nini, uangalie nini, uambatane na nani na ufanye nini.
Sasa kama unachagua kufikiria vitu vinavyokufanya ujisikie vibaya, unataka kumlaumu nani? Kama umechagua mwenyewe kusikiliza na kuangalia habari hasi, halafu unajisikia kukata tamaa na maisha, unataka kumlaumu nani? Kama umechagua kukaa na watu ambao hawana wanakoelekea, watu waliokata tamaa na maisha yao, na wewe unaanza kuona maisha yako hayana maana, unafikiri nani wa kulaumiwa?
Kama unajisikia vibaya, umekata tamaa na maisha au unakosa hamasa ya kuchukua hatua, anza kuangalia maamuzi uliyofanya kwenye maisha yako, na utaona jinsi yale uliyochagua wewe mwenyewe yanakuweka kwenye hali hiyo.
Na uzuri ni kwamba wewe ndiye unayechagua, hivyo usijaribu kumlaumu yeyote. Kama hupendi pale ulipo sasa badili kitu, wewe siyo mti kwamba lazima uendelee kuwa hapo ulipo sasa.



 Na  Mwl  Japhet  Masatu , Dar  es  salaam , Tanzania,  Afrika Ya  Mashariki ---Mwl  wa  Maisha Na  Mafanikio, Mshauri, Public Speaker(MC), Mwandishi, Mjasiriamali /
Tuwasiliane kwa :+ 255 755 400 128 / + 255 716 924136(WhatsApp ).  EMAIL: japhetmasatu@gmail.com

No comments:

Post a Comment