Tuesday, April 23, 2019

UKWELI KUHUSU UTAJIRI.

Wengi wanapoingia kwenye safari hii ya utajiri, huwa wanaona mambo mazuri tu mbele, kwamba wakishapata utajiri maisha yatakuwa mazuri na watakuwa na furaha.
Felix anatupa ukweli kuhusu utajiri, kupitia maisha yake binafsi, ili tuelewe ni kitu gani tunakwenda kukutana nacho mbele, na tujiandae vizuri.
Kwanza kabisa anasema utajiri haujawahi kumletea yeye furaha, zaidi umemletea matatizo makubwa ya kiafya baada ya kujihusisha na ulevi, madawa ya kulevya na uzinzi.
Pili anasema utajiri unakufanya uwe chambo ambapo kila mtu atatumia kila njia kupata fedha zako. Wapo watakaotumia njia za kuomba, wengine kuiba na hata wengine kukushitaki kwa kitu ambacho hujafanya.
Tatu utajiri utaharibu mahusiano mengi uliyonayo. Mahusiano ya ndoa, kwa wengi yanaathirika sana. mahusiano ya kifamilia na kindugu nayo yanaathiriwa sana na safari yako ya utajiri na hata baada ya kufikia utajiri.
Kwa kifupi kadiri unavyokuwa tajiri siyo kwamba matatizo uliyonayo yanaondoka, bali yanakuwa makubwa zaidi. Hivyo jiandae kukabiliana nayo, na kazana kujijengea busara zaidi kadiri unavyoendelea kutajirika. Kwa sababu utajiri bila busara utakuwa ni kujichimbia kaburi lako mapema.

No comments:

Post a Comment