Tuesday, April 23, 2019

KUWA KING"ANG"ANIZI NA MVUMILIVU UTAFANIKWA SANA.

Kila kitabu kinachohusu mafanikio kinasisitiza sana ung’ang’anizi na uvumilivu ili kuweza kufanikiwa. Lakini siyo kila ung’ang’anizi na uvumilivu utakufikisha kwenye mafanikio. Bali unahitaji ung’ang’anizi sahihi, na kukubali pale ambapo umekosea ili kuboresha zaidi.
Tunapaswa kuwa ving’ang’anizi ili kupata utajiri na mafanikio, tunapaswa kujaribu tena na tena na tena kila tunaposhindwa. Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba kufanya jambo lile lile kwa njia ile ile halafu kutegemea kupata matokeo tofauti ni maana sahihi ya ujinga.
Tunapaswa kung’ang’ana kwa njia sahihi, tunapaswa kubadili njia tunazotumia, ambacho hatupaswi kubadili ni lengo ambalo tumejiweka. Tunapaswa kuendelea na mapambano mpaka pale tutakapopata tunachotaka.
Wote tunajua jinsi ambavyo dunia ina uangalifu, haikubali kutoa kitu kwa mtu ambaye hajaonesha kweli anakitaka na yupo tayari kulipa gharama kukipata. Jioneshe kwamba wewe unautaka utajiri kweli, kuwa tayari kulipa gharama na ng’ang’ana kwa njia sahihi na utapata unachotaka.

No comments:

Post a Comment