Tuesday, April 23, 2019

SIKILIZA NA JIFUNZE.

Kusikiliza ndiyo silaha yenye nguvu sana katika safari ya mafanikio. Ukiwa msikilizaji mzuri, utajifunza mambo mengi sana kwa watu wengine. Kuanzia wale unaofanya nao kazi na hata wale ambao inabidi upatane nao kwenye makubaliano mbalimbali.
Kusikiliza ni kugumu sana, na wengi hawawezi kusikiliza kwa umakini ndiyo maana hawajifunzi, hawajui watu wanataka nini na kuweza kuwapatia. Ukiwa mtu wa kusikiliza kwa umakini, kwa lengo la kuelewa na kujifunza, utajua mengi na pia utazijua tabia za watu, ambazo utaweza kuzitumia kwa mafanikio zaidi.
Ukiwasikiliza wateja wako utayajua mahitaji yao hata kama hawajakuambia wazi na kuweza kuwatimizia. Ukiwasikiliza wafanyakazi wako utajua kinachowahamasisha na ukiwapatia watajituma zaidi. Ukiwasikiliza unaotaka kufikia nao makubaliano, utajia udhaifu wao uko wapi na kuweza kuutumia.
Katika safari ya mafanikio na utajiri, kusikiliza na kujifunza ni hitaji muhimu sana. Hata watu wanawaheshimu sana wale ambao wanachukua muda na kusikiliza. Tumia nguvu hii kwa manufaa yako na ya wengine pia.

No comments:

Post a Comment