Tuesday, April 23, 2019

KUWA NA VYANZO VINGI VYA KIPATO.

Chanzo kimoja cha kipato ni utumwa, iwe ni kazi au biashara, huwezi kutajirika kwa kutegemea chanzo kimoja pekee. Angalia matajiri wote wakubwa, hakuna hata mmoja ambaye anategemea chanzo kimoja pekee cha kipato.
Kila biashara huwa ina changamoto zake, hakuna biashara ambayo inafanya vizuri wakati wote, kila biashara kuna kipindi inafanya vizuri na kipindi kingine inafanya vibaya. Unapotegemea biashara moja pekee, kila wakati utakuwa kwenye kupanda au kushuka.
Dawa ya kuondoa hali hiyo ya kupanda na kushuka ni kuwa na vyanzo vingi vya kipato, na ambavyo havitegemeani. Hivyo unapokuwa na changamoto eneo moja, eneo jingine linakuwa linaenda vizuri.
Kanuni hii haiwahusu wale wanaoanza, unapokuwa unaanza, anza na kitu kimoja na kiwekee msingi imara wa kuweza kujiendesha chenyewe. Baada ya kuhakikisha kitu cha kwanza kimekuwa imara, hapo sasa unaweza kuanzisha kitu kingine. Kuanza vitu vingi kwa wakati mmoja ni njia ya uhakika ya kushindwa.

No comments:

Post a Comment