Tuesday, April 23, 2019

JIAMINI WEWE MWENYEWE.

Kama hujiamini wewe mwenyewe, hakuna yeyote anayeweza kukuamini na hutaweza kufanikiwa kwenye jambo lolote maishani mwako.
Unapaswa kujiamini wewe mwenyewe, unapaswa kuamini kwamba una uwezo mkubwa ndani yako wa kukuwezesha kupata chochote unachotaka, unapaswa kuamini hakuna kinachoweza kukuzuia kupata kile unachotaka. Tunaambiwa imani inaweza kuihamisha milima, na hii ndiyo imani unayopaswa kuwa nayo ili kufanikiwa na kufikia utajiri.
Katika safari yako ya kusaka utajiri utakutana na vikwazo vya kila aina, utapatwa na hofu nyingi, wapo watakaokukatisha tamaa kwa kukupa mifano ya wengi walioshindwa. Kitu pekee kinachoweza kukuvusha kwenye hali hizo ni kujiamini wewe mwenyewe.
Pia hakuna utakachopanga na kikaenda kama ulivyopanga, utashindwa kwenye mambo mengi licha ya kufanya kila unachopaswa kufanya. Kujiamini ndiyo kutakupa nguvu ya kuamka kila unapoanguka ili uweze kuendelea na safari ya mafanikio.
Jiamini wewe mwenyewe na hakuna kitakachoweza kukuzuia kufanikiwa.

No comments:

Post a Comment