Tuesday, April 23, 2019

JE, NI KWELI WALIOFANIKIWA WANA BAHATI ?


Felix Dennis katika kitabu chake anatuambia ni kweli kwamba watu waliofanikiwa wana bahati kuliko wale ambao hawajafanikiwa. Lakini kitu tunachopaswa kujua ni hiki, bahati hazikuwafuata vitandani kwao wakiwa wamelala. Bali walikutana na bahati katika mapambano yao.

Hivyo ili ufanikiwe unahitaji kupata bahati, lakini bahati hiyo haitakutafuta wewe, itabidi uitafute wewe. Lazima uweke kazi, lazima ujitume sana, na katika kujituma kwako ndiyo utakutana na fursa ambazo wengine hawawezi kuzitumia kwa sababu hawana maandalizi kama uliyonayo wewe.

Hivyo tunajumuisha kwa kusema, bahati ni pale maandalizi yanapokutana na fikra. Kama unataka bahati zaidi, hakikisha unakuwa na maandalizi bora zaidi.

No comments:

Post a Comment