Tuesday, April 23, 2019

AMINI SAUTI YAKO YA NDANI.

Kila mmoja wetu ana sauti iliyopo ndani yake, hisia fulani unazozipata ambazo huwezi kuzielezea, ambazo zinakuashiria kama kitu ni kibaya au kizuri, kama ni sahihi au siyo sahihi. Mara nyingi huwa tunapuuza sauti hii na matokeo yake tunafanya makosa makubwa. Kuna wakati ndani yako unapata msukumo wa kufanya au kutokufanya kitu, lakini ushawishi wa nje unakufanya uende kinyume na sauti hiyo na unakuja kugundua ungejisikiliza ungekuwa sahihi zaidi.
Jifunze kuamini sauti yako ya ndani, hata kama inaendana na uhalisia wa nje. Kuna kitu kwa nje kinaweza kuonekana ni sahihi, lakini sauti yako ya ndani ikakuambia siyo sahihi, au kitu kwa nje kikaonekana siyo sahihi, lakini sauti yako ya ndani ikakuambia ni sahihi. Jifunze kusikiliza sauti yako ya ndani, inajua zaidi kuliko wewe na itakuongoza kwa usahihi mara zote.
Watu wote ambao wamefikia utajiri na mafanikio makubwa, kuna hatua ambazo wamewahi kuzichukua, ambazo watu wa nje waliwaambia wanakosea, lakini wao walifanya, kwa sababu sauti ya ndani iliwaambia ndiyo kitu sahihi kufanya.
Unapojikuta njia panda na hujui hatua ipi sahihi kuchukua, isikilize sauti yako ya ndani, inajua njia sahihi na utaweza kufanya kilicho sahihi.

No comments:

Post a Comment