Friday, February 8, 2019

MVUTO NA USHAWISHI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.

Mvuto na ushawishi ni vitu viwili ambavyo kila anayetaka kufanikiwa na kutengeneza kipato kikubwa anapaswa kuwa navyo. Dean anaita vitu hivi viwili kichocheo cha utajiri, vikikosekana huwezi kufikia mafanikio makubwa na utajiri.
 
Mvuto na ushawishi ni njia nyingine ya kusema MASOKO NA MAUZO. Kila tunachofanya kwenye maisha ni masoko, na kila kinachotuingizia kipato ni mauzo.

Hivyo tunaweza kusema kazi zetu kubwa kwenye maisha ni mbili, MASOKO NA MAUZO. Tunapaswa kujiweka kwa njia ambayo watu wayajua uwepo wetu, na pia tuweze kuwashawishi watu hao kutupa kile ambacho tunataka watupe.

Katika kuboresha masoko na mauzo kwenye biashara zetu, kazi zetu na hata maisha yetu kwa ujumla, Mwandishi Dean anatushirikisha hatua zifuatazo za kuchukua;

------Kuwa muwazi na mwaminifu mara zote. Uaminifu unalipa.
------- Kuwa wewe na kuwa na hamasa, usijaribu kuingiza kuwa mtu mwingine.
--------Amini kwenye utele na siyo uhaba, amini kuna wingi wa chochote kwa ajili ya kila mtu.
------Wape watu kile wanachotaka na siyo wanachohitaji.
-----Tumia hadithi, watu wanaelewa na kusukumwa zaidi na hadithi na mifano kuliko maelezo pekee.
------Usiwe mwongeaji sana, ukishaeleweka nyamaza.
Kuwa na msukumo wa ndani wa kile unachofanya.
-------- Endelea kutengeneza mahusiano na wale ambao unawauzia au wameshakubaliana na wewe.
-----Tengeneza mtazamo wa shukrani.
-------Zingatia zaidi kujenga mahusiano kuliko kipato, fanya kile ambacho kitaboresha mahusiano yako na unayetaka kumuuzia au akubaliane na wewe.

No comments:

Post a Comment