Friday, February 22, 2019

KILA MTU ANA NGUVU YA MAFANIKIO MAKUBWA NDANI YAKE . ONDOA VIKWAZO VYA MAFANIKIO YAKO.

Kila mtu ana nguvu ya mafanikio ndani yake, kitu pekee anachopaswa kufanyia kazi ni kuondoa vikwazo vya mafanikio yetu. Vitu kama tabia zetu wenyewe, hisia zetu na mengine yanatuzuia tusifikie mafanikio ambayo tayari yapo ndani yetu.
Kwa kifupi, hakuna kikubwa tunachoweza kufanya kuyabadili mafanikio yaliyopo ndani yetu, ni makubwa sana, kinachotufanya tusiyafikie ni vikwazo tunavyotengeneza au kuruhusu viingie kwenye maisha yetu.
Kadhalika kwenye fedha na utajiri, kila mtu tayari ana utajiri ndani yake, kinachomzuia mtu kufikia utajiri wake ni vikwazo anavyokutana navyo au anavyotengeneza kwenye maisha yake.
Hivyo rafiki yangu, kila wakati jiulize swali hili, ni kikwazo gani nimeruhusu au kutengeneza kwenye maisha yangu ambacho kinanizuia kufikia mafanikio makubwa yaliyo ndani yangu?
Ukijiuliza swali hili na kujipa majibu sahihi, utaweza kuifanya safari yako ya mafanikio kuwa rahisi. Utaacha kujitesa na kujiumiza kwa vikwazo ulivyojiwekea au kuruhusu vikuzuie na utakuwa na mpango mzuri kwa mafanikio yako.
Tayari mafanikio unayo, unachohitaji ni kuondoa vikwazo vinavyoyazuia yasije kwako.
Moja ya njia za kuondoa vikwazo vya ukuaji kwako ni kujifunza kwa kujisomea vitabu.

No comments:

Post a Comment