Sunday, February 17, 2019

KULA MIMEA--NI SIRI YA KUISHI MIAKA ZAIDI YA 100.

Chakula chako kinapaswa kuwa mimea zaidi. Epuka kula nyama na vyakula vilivyosindikwa. Watu wengi walioishi miaka zaidi ya 100 sehemu kubwa ya chakula chao ni mimea. Nyama wanakula kwa kiwango kidogo sana na mara chache.
Ili kuongeza mimea zaidi kwenye vyakula vyako, zingatia mambo yafuatayo;
  1. Kula mbogamboga na matunda mara nne mpaka sita kwa siku. Kwa kila mlo wa siku, kuwa na matunda na matunda.
  2. Punguza ulaji wa nyama, kama unaweza acha kabisa, kama huwezi kula siyo zaidi ya mara mbili kwa wiki na kula kiasi kidogo cha nyama.
  3. Weka matunda sehemu ambayo ni rahisi kuyaona na kuyatumia unapokuwa unaendelea na shughuli zako. Hili litakusukuma kutumia matunda zaidi.
  4. Kula kunde zaidi. Vyakula vya jamii ya kunde vina virutubisho vya kutosha kwa mwili wako, fanya hivi kuwa sehemu kubwa ya chakula chako.
  5. Kula karanga kila siku, vyakula vya karanga na jamii yake, kama korosho na lozi vina mafuta mazuri kwa mwili wako na tafiti zinaonesha vinapunguza hatari ya magonjwa ya moyo.
  6. Kuwa karibu na karanga na vyakula vya jamii ya karanga ili iwe rahisi kwako kutumia mara kwa mara. Unaweza kuziweka kwenye chombo ambacho inakuwa rahisi kwako kutumia.

No comments:

Post a Comment