Friday, March 8, 2019

VIUNGO VYA UZAZI NI KITUO AMBACHO HUPOTEZA NGUVU NYINGI ZA WATU.

Kituo cha kwanza cha nguvu kipo kwenye viungo vyetu vya uzazi na kinadhibiti sehemu za mwili zilizopo chini ya kitovu. Hapa inahusika uke, uume, kibofu cha mkojo, sehemu ya mwisho ya utumbo na hata ngozi na misuli inayozunguka maeneo haya.
Kazi kubwa ya kituo hiki ni uzazi, jinsia, kujamiiana na kutoa uchafu mwilini. Homoni za uzazi huzalishwa kwenye kituo hiki. Kituo hiki kina nguvu kubwa sana ya ubunifu na uumbaji, fikiria nguvu ambayo inatumika katika kujamiiana na hata kupata mtoto.
Watu wengi wamekuwa wanatumia nguvu ya kituo hiki vibaya kwa kuelekeza nguvu zao nyingi kwenye kujamiiana na kuwa na mahusiano mengi ya kingono. Hili linawapunguzia uwezo wa kufanya makubwa kwenye maisha yao.
Ili uweze kutumia nguvu hii ya kituo cha kwanza katika kufanya miujiza, unapaswa kujidhibiti sana kwenye eneo la ngono, kwa kuwa hili ndiyo linapoteza nguvu za wengi.

No comments:

Post a Comment