Friday, March 8, 2019

TUMBO LA CHINI NI KITUO CHA NGUVU KWENYE MWILI KINAHUSU ULAJI WETU NA MAHUSIANO YETU NA WENGINE.

Tumbo la chini  ni   kituo  cha nguvu kwenye mwili hili ni eneo la mwili kwenye usawa wa kitovu. Kituo hiki kinadhibiti utumbo mpana, kongosho, kiuno, mifuko ya mayai na tumbo la uzazi kwa wanawake.
Kituo hiki kinahusika na ulaji, umeng’enyaji na utoaji wa mabaki ya chakula mwilini. Homoni mbalimbali huzalisha kwenye kituo hiki ambazo zinahusika na umeng’enyaji wa vyakula.
Kazi kubwa ya kituo hiki ni mahusiano ya kijamii, familia, utamaduni na hata mahusiano baina ya mtu mmoja na mwingine. Hiki ni kituo cha kushikilia au kuachilia au kuondoa.  Kituo hiki kinapokuwa vizuri, mtu unakuwa na utulivu na kujisikia salama na amani.
Watu wengi wamekuwa wanatumia nguvu ya kituo hiki vibaya kwa kuwa na hasira na vinyongo kwa wengine na kukosa maelewano mazuri na wengine. Kila unaposhikilia kitu ndani yako dhidi ya mtu mwingine, unashikilia nguvu ambayo ungeweza kuitumia kufanya makubwa kwenye maisha yako.
Ulaji uliopitiliza pia unaathiri kituo hiki kwa nguvu kubwa kutumika kumeng’enya chakula na kuondoa uchafu mwilini kitu ambacho kinazuia nguvu hiyo kutumika kwenye kutenda miujiza.
Ili kuweza kutumia vizuri nguvu ya kituo hiki, tunapaswa kudhibiti ulaji wetu na kuimarisha mahusiano yetu na wengine.

No comments:

Post a Comment