Saturday, March 9, 2019

TUMBO LA JUU NI ENEO LA NGUVU KWENYE MIILI YETU---KINAHUSIKA NA MATAKWA YETU,NGUVU ZETU ,UDHIBITI , HAMASA , MSUKUMO NA UTAWALA.

TUMBO  LA  JUU, ni   eneo   la  nguvu   kwenye   miili  yetu ,hili ni eneo la mwili juu ya kitovu. Kituo hiki kinadhibiti tumbo la chakula, utumbo mwembamba, bandama, ini, mfuko wa nyongo, figo na tezi zilizopo juu ya figo.
Kituo hiki kinahusika na matakwa yetu, nguvu zetu, udhibiti, hamasa, msukumo na utawala. Hiki ni kituo cha mashindano na nguvu binafsi, kujithamini na hata kuwatawala wengine.
Kituo hiki kinapokuwa vizuri, unaweza kutumia nguvu za kituo hiki kufikia malengo yako, kuwa na hamasa ya kupiga hatua zaidi na kuzivuka changamoto mbalimbali unazokutana nazo. Kituo hiki pia kinakupa nguvu ya kujilinda wewe mwenyewe na kuwalinda wale wa karibu kwako.
Watu wamekuwa wanatumia vibaya nguvu za kituo hiki kwa kujiona wao ni wa muhimu kuliko wengine, kutaka kuwatawala wengine na hata kuwaonea wengine pale mtu anapokuwa na mamlaka au nguvu fulani.
Kutumia vizuri nguvu za kituo hiki tunapaswa kujijua sisi wenyewe na kujua nini hasa tunachotaka kisha kuweka nguvu zetu kwenye maeneo hayo. Hatupaswi kujionesha kwa wengine au kuwalazimisha wengine wawe kama tunavyotaka sisi.

No comments:

Post a Comment