Thursday, March 21, 2019

LIPE TATIZO LAKO MUDA KAMA NJIA ZINGINE ZIMESHINDIKANA.

Wenye busara walisema muda ni tiba ya kila kitu. Kwamba hakuna kitu ambacho muda haukiathiri, hivyo kama kuna kitu kinakusumbua, ambacho unaona kimekushinda, uachie muda ufanye kazi yake.
 
Hakuna kitu ambacho muda unakiacha jinsi ulivyo bila ya kukiathiri, kadiri muda unavyokwenda, tatizo linakosa nguvu au njia bora za kulitatua inapatikana.
 
Hata kama kwa sasa huoni kabisa namna ya kuvuka ugumu unaopitia, usikate tamaa, jua muda uko upande wako. Unachohitaji ni uvumilivu na kusahau tatizo hilo kwa muda, kwa kutoruhusu likutawale wakati huna cha kufanya.
 
Kila ugumu unaopitia, jua kwamba utaupatia jawabu au muda utatoa jawabu. Hivyo kama umeshafanya kila unachoweza kufanya na zaidi, lakini hupati majibu, hapo siyo mwisho, muda una nafasi kubwa ya kuhangaika na tatizo hilo. Kubali na songa mbele na mengine yaliyo ndani ya uwezo wako, na muda utahangaika na hilo lililokushinda.

No comments:

Post a Comment