Sunday, March 24, 2019

ENEO LA UBUNIFU :Ulipo Sasa, Unakotaka Kufika, Viwango vya Kujiwekea, Kitabu Cha Kujisomea.

Unapaswa kuwa na kitu cha kibunifu unachofanya kwenye maisha yako. Kitu hiki kinachochea akili yako kufikiri zaidi na kukuwezesha kukua zaidi. Inaweza kuwa uandishi, uchoraji, uimbaji, upigaji vifaa vya muziki, uigizaji na kadhalika.
ULIPO SASA; je unaamini kwamba wewe ni mbunifu? Je kuna mtu mbunifu ambaye unapenda sana kuwa kama yeye? Ni mambo gani ya kibunifu ambayo unafanya sasa kwenye maisha yako? Je ni vipaji gani ulivyonavyo na unavitumiaje?
UNAKOTAKA KUFIKA; ni ubunifu gani ambao ungependa kuwa nao na kubobea zaidi siku zijazo? Ni jinsi gani unaweza kutumia ubunifu huo kuwasaidia wengine zaidi. Chagua ubunifu unayotaka kuwa nao na jiendeleze kila siku na kutoa mchango kwa wengine.
VIWANGO VYA KUJIWEKEA; chagua aina ya ubunifu ambao utakuwa unajihusisha nao na kila siku tenga muda wa kujiendeleza kwenye ubunifu huo. Unaweza pia kujiunga na wengine au kushiriki madarasa yanayokuwezesha kukuza zaidi ubunifu wako.
KITABU CHA KUSOMA; soma kitabu THE WAR OF ART cha Steeven Pressfield ambacho kitaamsha na kuchochea ubunifu uliopo ndani yako na kuweza kufanya kazi za kibunifu.

No comments:

Post a Comment