Sunday, March 24, 2019

ENEO LA KAZI : Ulipo Sasa, Unakotaka Kufika, Viwango Vya Kujiwekea , Kitabu Cha Kusoma.

Kazi au biashara unayofanya ni eneo muhimu sana la maisha yako. Hili ni eneo ambalo unapaswa kuwa unakua kadiri muda unavyokwenda. Kwa sababu kubaki pale pale, ni kurudi nyuma. Katika kazi au biashara unayofanya, lazima uweze kupima ukuaji wako.

ULIPO SASA; unaielezeaje kazi? Je unafurahia kazi au biashara unayoifanya? Je unajiona kuwa kwenye nafasi ya kufanikiwa kupitia kazi au biashara unayofanya. Je unakua kwa kiasi gani ukijipima kikazi na kibiashara?

UNAKOTAKA KUFIKA; ni ubobezi gani unajiona kuwa nao kwenye kazi unayofanya? Ni mabadiliko gani ungependa kuleta kupitia kazi au biashara unayofanya. Kuwa na picha ya mchango wako mkubwa na mabadiliko unayotaka kuleta na ifanyie kazi kila siku.

VIWANGO VYA KUJIWEKEA; jiunge na kundi la kitaalamu kulingana na taaluma au ujuzi ulionao. Shiriki mikutano na mafunzo mbalimbali yanayoendana na taaluma na ujuzi ulionao. Pia jipime jinsi unavyokua kupitia kazi au biashara unayofanya.

KITABU CHA KUSOMA; kitabu ORIGINALS cha Adam Grant ni kitabu kitakachokuwezesha kuwa na ubunifu mkubwa kwenye kazi yako na kufikiria nje ya boksi, kuuza mawazo yako na kuleta mapinduzi.

No comments:

Post a Comment